BOBI WINE ACHUKUA FORM YA URAIS CHAMA CHA NPU NCHINI UGANDA

Kiongozi wa chama cha National Unity Platform (NUP) Robert Sentamu Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine, hapo jana alichukuliwa fomu ya urais ya uchaguzi mkuu utakaofanyika Januari, 2026 nchini Uganda.

Kiongozi wa upinzani bungeni Joel Ssenyonyi , Katibu Mkuu wa chama David Rubongoya na Msimamizi wa Hazina ya Kitaifa ya chama Benjamin Katana walichukua fomu kwa niaba ya Kyagulanyi kutoka makao makuu ya Tume ya Uchaguzi.


Chama cha NUP kilisema kitafanya kampeni zake chini ya kauli mbiu, ‘’Uganda Mpya Sasa’’ na kuongeza kuwa hilo litafikiwa kwa upigaji kura wa kiwango cha juu.



‘’Uganda mpya tunayozungumzia ni nchi ambayo watu wote wakuwa wanakwenda kwenye hospitali za umma na kupata matibabu mazuri, barabara zetu ziwe katika hali nzuri, mahali ambapo watoto wetu wanakwenda shule kupata elimu bora,’’ Ssenyonyi aliambia vyombo vya habari.


Hii itakuwa mara ya pili kwa Robert Kyagulanyi kugombea urais dhidi ya Rais Yoweri Museveni.


Mwaka 2021, alimaliza kinyang’anyiro hicho katika nafasi ya pili kwa kupata kura 3,475,398 sawa na asilimia 34.83 ya kura zote.

Share: